BABU OWINO ASHUTUMU UBOMOAJI GIKOMBA
Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino ameshutumu vikali uboaji wa makazi katika mtaa wa Gikomba jijini Nairobi
Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Owino ameutaja ubomoaji huo kuwa wa kinyama na usiozingatia maslahi ya wamiliki wa biashara ndogo ndogo.
Aidha, mbunge huyo amemtaka rais William Ruto kuwapa waathiriwa wa Gikomba hifadhi kwenye makazi ya bei nafuu yanayojengwa na serikali.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































