#Local News

USHURU WA MKATE WATUPILIWA MBALI

Serikali ya Kenya Kwanza imetupilia mbali mapendekezo makuu ya ushuru ambayo yamezua taharuki miongoni mwa Wakenya

Tangazo hilo linajiri baada ya Rais William Ruto kuandaa mkutano wa kundi la wabunge katika Ikulu ya Nairobi hii leo

Katika kikao na wanahabari baada ya mkutano wa PG, wandani wa rais Ruto wamesema mapendekezo hayo yametupiliwa mbali kufuatia zoezi la ushirikishwaji wa umma ambalo lilishuhudia Wakenya wakiibua upinzani dhidi yao

Miongoni mwa mapendekezo yaliyorekebishwa ni ushuru wa mkate, gari na ushuru wa mazingira

Imetayarishwa na Janice Marete

USHURU WA MKATE WATUPILIWA MBALI

“ASANTE, LAKINI HAPANA!” WAKENYA WAJIBU

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *