#Football #Sports

WACHEZAJI 22 WAREJEA NDANI YA CITY

Nairobi City Stars imethibitisha kuwa wachezaji 22 kati ya 28 wa muhula uliopita watarejea kikosini huku timu ikijiandaa kwa msimu wa Ligi Kuu ya FKF wa 2024/2025

Wachezaji sita kati ya 22 walikuwa na kandarasi za kukimbia, huku wengine 16 wakiongeza kusalia kwao kwa msimu mwingine ambao utaanza tarehe 24-25 Agosti 2024 kwa mchezo wa ugenini dhidi ya Kenya Police FC.

Mlinda mlango Elvis Ochoro atakuwa anaamilisha mwaka wa tano na wa mwisho wa kandarasi yake huku beki wa kati Wycliffe Awiko Omondi, pamoja na mlinda ndege Gilbert Abala, wakiingia mwaka wao wa pili.

Kiungo Vincent Owino, beki wa kati Timothy Muganda, na beki wa kushoto Rogers Wasega wanakamilisha orodha ya wachezaji walio na kandarasi za kukimbia.

Walinda mlango Edwin Mukolwe na Byron Owino ni sehemu ya 16 walioongeza kandarasi zao na watasalia kwa msimu ujao.

Kiungo wa kati Clifford Ouma yuko katika msimu wake wa tatu mfululizo huku Elvis Noor Ojiambo akikubali kusalia Simba wa Nairobi kwa msimu wake wa sita.

Ouma na Noor watakuwa na viungo Brian Mzee na Abuyeka Kubasu, ambao pia watapamba msimu mwingine.

Imetayarishwa na Nelson Andati

WACHEZAJI 22 WAREJEA NDANI YA CITY

HATUJALIPWA PESA ZETU

WACHEZAJI 22 WAREJEA NDANI YA CITY

BWAKE WATAWAZWA WASHINDI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *