RUTO AENDELEA KUAHIDI NYUMBA
Rais William Ruto ameahidi kuwa serikali yake itawajengea nyumba 40,000 chini ya mpango wa makazi ya bei nafuu wakazi wa Nairobi waliopoteza makazi yao kufuatia mafuriko.
Akizungumza mtaani Kibra ambako amezuru kukagua ujenzi wa mradi huo, Ruto amesema kandarasi ya ujenzi wa makazi hayo itatolewa hivi karibuni kwa lengo la kuhakikisha watu waliohamishwa na serikali kutokana na mafuriko wanapata makazi.
Aidha, amesema kwamba kuna zaidi ya nyumba 110,000 kote nchini ambazo zinaendelea kujengwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































