KNUT YASHINIKIZA MASLHAI BORA KWA WALIMU WA BONI

Muungano wa walimu wa shule za msingi KNUT umeshinikiza serikali kuangazia na kutimiza matakwa ya walimu wanaofunza kwenye shule zilizo ndani ya msitu wa Boni.
Walimu hao wanamtaka mwajiri wao TSC kuwapandisha vyeo na kuwapa marupurupu ya kufanya kazi katika mazingira magumu.
Aidha, wamelalamikia kudhoofika kwa wenzao kiafya kutokana na mazingira magumu wanamofanyia kazi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa