MUITE ANATAKA KESI ZA KUPINGA KUONDOLEWA KWA GACHAGUA ZIPELEKWE KWA JAJI MKUU MARTHA KOOME

Wakili Paul Muite, wakili mkuu wa Naibu Rais Rigathi Gachagua anataka kesi zinazopinga kuondolewa kwa mteja wake ziwasilishwe mbele ya Jaji Mkuu Martha Koome kuunda benchi ya majaji watatu kuzisikiliza.
Kwa mujibu wa Muite masuala yaliyo mbele ya Jaji Lawrence Mugambi yanaibua masuala mazito.
Muite anasema Kifungu cha 1 cha katiba ni muhimu sana na mahakama inafaa kuzingatia na kwamba kifungu hicho kinazungumzia uhuru wa watu waliomchagua rais na naibu wake.
Imetayarishwa na Janice Marete