#Local News

WALIMU 20,000 KUAJIRIWA MWAKANI, RUTO AAHIDI

Shughuli za masomo zinatarajiwa kuimarika zaidi kuanzia Januari mwaka ujao baada ya Rais William Ruto kufichua kwamba serikali ina mpango wa kuwaajiri walimu 20,000 zaidi kuhakikisha kuwa wanafunzi nchini wanapokea elimu bora.

Akizungumza katika Ikulu ya Nairobi, Rais amewataka wazazi kuwekeza pakubwa katika elimu ya wanao, huku serikali ikijizatiti kuwaajiri walimu zaidi.

Aidha, amewahakikishia watahiniwa wa KCSE na KPSEA usalama wao wanapojiandaa kwa mitihani yao.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WALIMU 20,000 KUAJIRIWA MWAKANI, RUTO AAHIDI

GACHAGUA: CHECHE ZACHACHA SENETI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *