AJALI KAKAMEGA: FAMILIA YAOMBOLEZA JAMAA 2

Familia moja katika eneo la Sabatia kaunti ya Vihiga inaomboleza kifo cha jamaa zao wawili walioangamia kwenye ajali hapo jana jioni katika eneo la Iguhu, idadi ya watu waliofariki hadi sasa ikiwa 10.
Kwa mujibu wa familia hiyo, jamaa zao walikuwa safarini kutoka kwenye sherehe ya kifamilia katika eneo la Soy, wawili wakiangamia papo hapo huku wengine 4 wakiendelea kupokea matibabu.
Wameitaka serikali kuwasaidia kugharamia matibabu ya waathiriwa na mipango ya mazishi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa