SIWALIPI, GAVANA LUSAKA KWA WANAKANDARASI

Wanakandarasi wanaojenga madarasa ya chekechea kwenye kaunti ya Bungoma wameonywa dhidi ya kufanya kazi duni kwenye ujenzi huo, hatua ambayo inahatarisha maisha ya wanafunzi.
Akizungumza katika eneo bunge la Bumula, gavana wa Bungoma Ken Lusaka ameonya kuwa serikali yake italazimika kukosa kuwalipa wankandarasi wanaokosa kuafikia viwango hitajika vya ujenzi.
Amezungumza wakati wa uzinduzi wa usambazaji wa vifaa vya masomo katika shule za chekechea.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa