WAHUDUMU WA UHC WAENDELEZA MGOMO NORTHRIFT

Huduma za matibabu katika vituo mbali mbali vya afya kwenye kaunti zote 7 za Northrift zimeendelea kusambaratika kufuatia mgomo unaoendelea wa wahudumu wa afya walioajiriwa chini ya mpango wa afya kwa wote UHC, ambao wamekongamana mjini Kapsabet kaunti ya Nandi kufanya maandamano.
Wahudumu hao wanashinikiza kuajiriwa kwa kanadarasi ya kudumu, wakidai kwamba serikali imewapuuza.
Wameapa kutorejea kazini hadi malalamishi yao yatakaposhughulikiwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa