NCHI TANO ZAJIANDAA KWA MICHUANO YA NDONDI
Nchi tano zimethibitisha kushiriki katika mashindano ya kimataifa ya ndondi ya ‘Challenge Omar Bongo Ondimba’ yaliyopangwa kufanyika Libreville, Gabon kuanzia Mei 30-Juni 11.
Nazo ni Congo Brazzaville, Cameroon, Angola, Zimbabwe, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Tarehe ya mwisho ya usajili, iliyopangwa awali Aprili 28, imeongezwa hadi Mei 16, 2025.
PESA ZA ZAWADI zitatolewa kwa washindi wote wa medali za dhahabu, fedha na shaba.
Washindi wa medali za dhahabu watapata $1,600, fedha $1,300 na shaba $800.
Imetayarishwa na Nelson Andati
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































