#Local News

SHUGHULI ZAVURUGIKA KWENYE KIWANDA CHA NZOIA KUFUATIA MAANDAMANO

Shughuli katika kiwanda cha sukari cha Nzoia zimetatizika baada ya wafanyakazi kuandamana kupinga ubinafsishaji wa kiwanda hicho.

Wafanyikazi hao aidha wanasema kuwa hawatakubali usimamizi mpya kabla ya kulipwa mishahara yao yote, wakidai serikali inapuuza maslahi yao na sheria za ajira licha ya huduma yao ya muda mrefu.

Inaarifiwa kuwa tayari serikali imekamilisha mchakato wa kubinafsisha kiwanda hicho

Imetayarishwa na Janice Marete

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *