#Sports

BARCELONA WAREJEA UWANJANI CAMP NOU

Barcelona wametangaza kurejea kwao Camp Nou mpya kwa ajili ya mechi ya kirafiki Agosti 10 baada ya kazi ya miaka mingi ya kupanua na kuufanya uwanja huo kuwa wa kisasa.

Mechi ya jadi ya kujiandaa na msimu mpya ya Joan Gamper Trophy itaashiria kufunguliwa tena kwa uwanja, huku kazi ya ujenzi ikiendelea katika maeneo mbalimbali, mabingwa hao wa sasa wa Uhispania walisema katika taarifa.

Miamba hao wa Kikatalani hawajathibitisha uwezo wao wa awali, lakini vyombo vya habari vya ndani viliripoti kwamba stendi zilizopo zinaweza kubeba mashabiki 35,000.

Baada ya kucheleweshwa mara kadhaa tangu kuanza kwa 2023, mradi uliopewa jina la “Espai Barca” unatarajiwa kukamilika katika msimu wa joto wa 2026 na kuongeza uwezo wa Camp Nou hadi viti 105,000.

Barcelona kwa wakati huu wamecheza mechi zao za nyumbani kwenye uwanja mdogo wa Olimpiki wa Montjuic.

Kylian Mbappe alianza tena mazoezi na wachezaji wenzake wa Real Madrid siku ya Jumatano baada ya kupata nafuu kutokana na ugonjwa wa gastroenteritis, kabla tu ya mchezo wa Kundi H wa timu yake kwenye Kombe la Dunia la Klabu dhidi ya RB Salzburg.

Fowadi huyo wa Ufaransa alilazwa kwa muda mfupi katika hospitali ya eneo la Miami wiki iliyopita na akakosa mechi mbili za kwanza za Real, sare ya 1-1 dhidi ya Al-Hilal na ushindi wa 3-1 dhidi ya Pachuca.

Real wanaongoza Kundi H wakiwa na pointi nne, mbele ya RB Salzburg kwa tofauti ya mabao na Al-Hilal, ambao bado wanaweza kufuzu kwa awamu ya muondoano, wakiwa na pointi mbili kwa sasa.

Imetayrishwa na Nelson Andati

BARCELONA WAREJEA UWANJANI CAMP NOU

CAMILO AAGA DUNIA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *