UCHUNGUZI WAANZISHWA KWENYE MKASA WA NDEGE KIAMBU
Vikosi mbali mbali vya usalama vinanendeleza uchunguzi katika mkasa wa ndege ya shirika la Amref iliyoanguka hapo jana katika eneo la Mwihoko kaunti ya Kiambu, na kusababisha vifo vya watu 6.
Ndege hiyo ndogo iliyokuwa ikitoka uwanja mdogo wa ndege wa Wilson jijini Nairobi kuelekea Hergeisa nchini Somalia, iliangukia nyumba kadhaa mtaani humo muda mfupi baada ya kupaa angani.
Kamishna wa kaunti ya Kiambu Henry Wafula, amesema serikali itafanya uchunguzi wa kina kuibaini chanzo cha ajali hiyo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































