WAATHIRIWA WA MAANDAMANO WANUSIA FIDIA
Rais William Ruto ametangaza mpango wa kuwafidia raia na maafisa wa usalama waliojeruhiwa wakati wa maandamano kuanzia mwaka wa 2017 hadi sasa.
Kupitia agizo la rais, Ruto amesema mpango huo unalenga kuleta usawa kuhusiana na uhuru wa kikatiba na majukumu ya raia, huku ikiangazia hasara ya kiuchumi inayosababishwa na maandamano ya kisiasa.
Mpango huo unaoongozwa na mshauri wake mkuu kuhusu masuala ya kikatiba Professa Makau Mutua, utadumu kwa kipindi cha siku 120.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































