KIGAME ATAZAMIA URAIS
Kinyang’anyiro cha urais kwenye uchaguzi mkuu ujao kimeendelea kushika kasi na kuwavutia wawaniaji mbali mbali, wa hivi punde akiwa ni mwimbaji wa nyimbo za injili Reuben Kigame.
Akitangaza kujitosa kwenye kinyang’anyiro hicho, Kigame aliyezuiwa kuwania kwenye uchaguzi mkuu uliopita, amesema atatota suluhu kwa matatizo yanayolikumba taifa kama vile ufisadi iwapo atachaguliwa kuwa rais.
Ameisuta serikali ya Kenya Kwanza kwa madai ya kushindwa kutekeleza ahadi ilizotoa kwa wakenya.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 






































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































