MSAKO WAIMARISHWA NAIROBI
Washukiwa wa wizi wa kimabavu zaidi ya 300 jijini Nairobi ambao wamekamatwa kufikia sasa wanatarajiwa mahakamani hii leo kufunguliwa mashtaka mbali mbali, baada ya kukamatwa wakati wa operesheni maalum iliyoagizwa na serikali.
Polisi wamewataka waathiriwa wa uhalifu huo katikati mwa jiji la Nairobi kuandikisha taarifa ili kusaidia katika uchunguzi na kufanikisha mashtaka dhidi ya washukiwa.
Wakati uo huo, gavana wa Nairobi Johnson Sakaja, amewahakikishia wakazi usalama kwa ushirikiano na polisi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































