SOFAPAKA WACHANA BARUA ZA POSTA
Klabu ya Sofapaka ilipata ushindi muhimu wa ligi kwa kuicharaza Posta Rangers mabao 2-0 hapo jana kwenye uwanja wa Dandora jijini Nairobi.
Wachezaji Daniel Nganga na Josesph Kuloba, waliwafungia Batoto ba Mungu mabao hayo muhimu na kuwapa pointi 3 ambazo zinawaweka katika nafasi ya 7 kwa pointi 11, 5 nyuma ya vigogo Gor Mahia kwenye msimamo wa ligi kuu KPL.
Katika mechi za National Super League, Mombasa United waliendeleza msururu wa matokeo bora kwa kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Darajani Gogo.
Eric Adem aliwafungia Gogo kabla ya Neville Amwai kufunga bao la ushindi kwa wenyeji baada ya mchezaji wa Gogo kujifunga.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































