KENYA YAPUZILIA MBALI VITISHO VYA MUSEVENI
Wizara ya masuala ya kigeni nchini imepuzilia mbali vitisho vya rais wa Uganda Yoweri Museveni kuhusu nia yake ya kuinyakua bandari ya Mombasa na Bahari Hindi katika eneo la Kenya, ikisema Museveni ana ufahamu kuhusu sheria za kimataifa kuhusu mipaka ya mataifa.
Akijibu maswali ya wanahabari, katibu mkuu katika wizara hiyo Korir Sing’oei, ameshikilia kuwa kauli ya Musaveni haina uzito.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































