RUTO: RIPOTI YA DHULUMA ITAZINGATIWA
Rais William Ruto ametoa hakikisho kuwa serikali itachukua hatua mwafaka kuhusu mapendekezo ya ripoti ya jopokazi la kiufundi kuhusu dhuluma za kijinsia nchini yakiwemo mauaji dhidi ya wanawake.
Akitoa hakikisho hilo, Rais amesema mapendekezo hayo yanahitaji hatua za haraka kuchukuliwa, akisema wanawake na wasichana ndio waathiriwa wakubwa wa dhuluma za kijinsia licha ya jinsia zote kuathirika.
Jopokazi hilo linaloongozwa na aliyekuwa naibu jaji mkuu Nancy Barasa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 









































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































