KAMERA BARABARANI KUDHIBITI AJALI
Jumla ya watu 5,000 waliaga dunia mwaka jana pekee wa 2025 kutokana na ajali za barabarani, ikiwa ni idadi ya juu zaidi ikilinganishwa na mwaka 2024.
Haya ni kulingana na ripoti iliyokabidhiwa Rais William Ruto, ambaye amesema kamera zitawekwa barabarani ndani ya mwezi mmoja ujao ili kuwanasa wanaokiuka sheria za trafiki, ikiwa ni sehemu ya mbinu za kukabili visa vya ajali nchini.
Kulingana na Rais, wakiukaji wa sheria watotozwa faini za papo hapo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































