SERIKALI: KATIBA IREKEBISHWE KUOKOA UCHUMI
Serikali sasa imependekeza marekebisho ya katiba ili kupunguza gharama ya serikali pamoja na mzigo mkubwa wa mishahara ya wafanyakazi wa umma.
Akiwa mbele ya kamati ya bunge kuhusu masuala ya bajeti, Waziri wa fedha John Mbadi, ameibua hofu kwamba huenda uchumi wa nchi ukashindwa kumudu gharama ya juu ya serikali, akisema katika mapendekezo ya bajeti ya shilingi trilioni 4.7 ya mwaka ujao wa kifedha, kiwango kikubwa kitatumika kulipia mishahara.
Ameyataka mabunge kufanyia katiba marekebisho.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































