#Football #Sports

MAGUIRE AENDELEZA MKATABA MANCHESTER UNITED

Nahodha wa zamani wa Manchester United, Harry Maguire, amesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja na klabu hiyo, ukiwemo uwezekano wa kuongeza mwaka mwingine.

Maguire mwenye umri wa miaka 33, ambaye mkataba wake wa sasa ungeisha mwishoni mwa msimu huu, aliungana na Manchester United kutoka Leicester City mwaka 2019 kwa kiasi cha paunmilioni 80, rekodi ya dunia kwa beki.

Kwa sasa amecheza mechi 266 kwa klabu hiyo na kushinda Kombe la Ligi msimu wa 2022-23 na Kombe la FA msimu uliofuata.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *