MUTULA AMKOSOA DUALE KUHUSU KAULI ZA NGAMIA
Gavana wa Makueni Mutula Kilonzo Jr amemkosoa Waziri wa Afya Aden Duale kufuatia matamshi yake kuhusu ngamia wanaotoka Garissa kuharibu mimea katika maeneo ya Ukambani.
Mutula amesema kauli hizo hazifai kutolewa na kiongozi wa kitaifa, hasa wakati ambapo kuna mvutano wa kiusalama katika eneo la Mwingi kati ya wafugaji wa ngamia na wakulima.
Amesisitiza kuwa viongozi wanapaswa kutafuta suluhu ya amani na kulinda maslahi ya wananchi badala ya kutoa matamshi yanayoweza kuchochea migogoro zaidi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































