#Football #Sports

ARSENAL WATWAA UBINGWA WA EPL BAADA YA MIAKA 22

Arsenal hatimaye wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi kuu ya Uingereza baada ya kusubiri kwa miaka 22, kufuatia sare ya 1-1 baina ya Manchester City na Bournemouth.

Matokeo hayo yamewafanya Arsenal kuhitimisha msimu wakiwa kileleni, na kukata ukame wa mataji uliodumu kwa miaka sita chini ya kocha Mikel Arteta.

Timu hiyo imekuwa na msimu imara, ikiwa imepoteza mchezo mmoja tu hivi karibuni na kushinda michezo minne mfululizo bila kuruhusu bao, hatua iliyowawezesha kutwaa ubingwa mapema.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *