#Local News

HUDUMA ZA USAFIRI ZAREJEA BAADA YA MGOMO KUSITISHWA

Ni afueni kwa wasafiri baada ya huduma za usafiri kurejea kote nchini kufuatia kusitishwa kwa mgomo wa kupinga ongezeko la bei ya mafuta.

Magari ya uchukuzi wa umma yalianza tena kubeba abiria kuanzia Jumanne alasiri baada ya serikali na wadau wa sekta ya usafiri kufikia makubaliano ya kuendelea na mazungumzo kwa muda wa siku saba kutafuta suluhisho la mzozo huo.

Wahudumu wa usafiri pia wamekubaliana kutoongeza nauli kwa sasa huku mazungumzo kuhusu bei mpya ya mafuta yakiendelea.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *