KINDIKI ASIFIA SEKTA YA USAFIRI KUSITISHA MGOMO
Naibu Rais Kithure Kindiki ameisifu sekta ya usafiri wa umma kwa kuitikia wito wa serikali wa kusitisha mgomo wa kitaifa uliokuwa umepangwa.
Kindiki amesema hatua hiyo imeleta afuweni kwa wananchi waliokuwa wakikabiliwa na changamoto za usafiri katika maeneo mbalimbali nchini.
Aidha, Naibu Rais ameahidi kuwa serikali itaendelea kuchunguza njia zote zinazowezekana ili kupunguza gharama ya mafuta na kupunguza mzigo wa maisha kwa wananchi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































