#Local News

MALI YAHARIBIWA WAKATI WA MAANDAMANO YA BEI YA MAFUTA

Mali ya thamani isiyojulikana imeharibiwa katika maeneo mbalimbali nchini baada ya wahuni kutumia maandamano ya kupinga ongezeko la bei ya mafuta kuvamia na kupora biashara.

Katika eneo la Naivasha, watu wawili walifariki baada ya polisi kufyatua risasi kwa kundi la watu waliokuwa wakivamia maduka na biashara.

Huko Murang’a, benki na maduka ya jumla yalivunjwa huku wakazi wakieleza matukio hayo kama mashambulizi yaliyopangwa na makundi ya kihalifu yaliyojipenyeza katika maandamano hayo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *