#Local News

NPS YAPINGA HABARI ZA KUKAMATWA KWA OCS WA NAIROBI CENTRAL

Huduma ya Kitaifa ya Polisi imekosoa taarifa zilizosambaa kuhusu kukamatwa kwa OCS wa Nairobi Central Dishen Ongoya, zikizitaja kama za upotoshaji.

Katika taarifa yake, msemaji wa polisi Muchiri Nyaga amesema madai hayo yaliyosambaa mitandaoni si ya kweli na hayapaswi kuaminika.

Hata hivyo, taarifa hizo zimezua mjadala baada ya ripoti za awali kuashiria kuwa afisa huyo alikuwa amezuiliwa na polisi.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *