#Local News

OMOLLO AKATAA WITO WA KUJIUZULU

Katibu mkuu katika Wizara ya usalama wa ndani Raymond Omollo amekataa wito wa baadhi ya viongozi wa upinzani wanaomtaka ajiuzulu, akisema hakuna msingi wa hatua hiyo.

Akizungumza katika mahojiano na kituo kimoja humu nchini, Omollo amesema madai hayo yanatokana na siasa na si ukweli wa mambo, akisisitiza kuwa anaendelea kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Wito wa kujiuzulu kwake umechochewa na ongezeko la matukio ya vurugu na mashambulizi dhidi ya mikutano ya kisiasa ya upinzani nchini.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *