#Local News

SERIKALI YATAKA HATUA DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA

Wizara ya Jinsia, Utamaduni na Huduma kwa Watoto imetoa wito wa kuchukuliwa kwa hatua za haraka kukabiliana na ongezeko la ukatili wa kijinsia na dhuluma dhidi ya watoto nchini.

Waziri Hannah Cheptumo amesema Kenya ilirekodi visa 10,531 vya dhuluma dhidi ya watoto kati ya Januari mwaka jana na Machi mwaka huu.

Amesema serikali na jamii lazima zishirikiane kulinda watoto na kukomesha vitendo vya ukatili.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *