#Football #Sports

MBIO ZA KUPANDA LIGI KUU ZAPAMBA MOTO NSL

Mbio za kupanda moja kwa moja hadi Ligi Kuu ya FKF zimezidi kupamba moto katika Ligi ya Taifa Daraja la Kwanza huku timu tatu zikifungana kileleni zikiwa zimesalia mechi tano pekee.

3K FC, Migori Youth na Mombasa United zote zina alama 68 baada ya kucheza mechi 33, huku 3K FC wakiongoza kwa tofauti ya mabao.

Kwa kuwa kuna alama 15 pekee zilizosalia kuwania, makosa yoyote katika mechi zilizobaki yanaweza kuamua nani atapanda ligi kuu msimu ujao.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *