#Local News

NAULI ZAPANDA LICHA YA MAZUNGUMZO

Wasafiri kote nchini wanakabiliwa na gharama kubwa za usafiri baada ya nauli kupanda licha ya wadau wa sekta ya matatu kuahidi kutopandisha bei wakati mazungumzo yanaendelea.

Hapa  jijini Nairobi baadhi ya nauli zimeongezeka kwa hadi asilimia 50 kufuatia matamshi ya awali ya waendeshaji wa usafiri wa umma.

Serikali imetakiwa kushughulikia suala la bei ya mafuta huku baadhi ya viongozi wakisema linaongeza gharama ya maisha na kuathiri uchumi pamoja na familia nyingi.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *