#Local News

ORENGO ASEMA MAISHA YAKE YAKO HATARINI

Gavana wa kaunti ya Siaya James Orengo amesema maisha yake yako hatarini baada ya serikali kuondoa walinzi wake bila maelezo.

Akizungumza na kituo kimoja humu nchini, Orengo amesema Inspekta Jenerali wa Polisi anapaswa kuwajibika iwapo jambo lolote litamtokea.

Orengo amesema maafisa wake tisa wa usalama waliokuwa wakimhudumia katika kaunti za Siaya na Nairobi waliondolewa ghafla Jumatano jioni bila sababu kuelekezwa kwake.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *