RUTO ATANGAZA PUNGUZO LA BEI YA DIESEL KUANZIA MWEZI UJAO
Rais William Ruto ametangaza kuwa bei ya dizeli itapungua kwa shilingi 10 kwa lita katika marekebisho yajayo ya bei ya mafuta ya Juni–Julai.
Akihutubia taifa kutoka Ikulu ya Mombasa, Rais amesema hatua hiyo inalenga kupunguza makali ya gharama ya maisha kwa wananchi, wafanyabiashara na sekta ya usafiri.
Amesema serikali tayari imetumia shilingi bilioni 13.7 katika kudhibiti bei ya mafuta kufuatia mzozo wa kimataifa uliosababisha kupanda kwa gharama za mafuta duniani.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































