#uncategorized

RUTO ATANGAZA PUNGUZO LA BEI YA DIESEL KUANZIA MWEZI UJAO

Rais William Ruto ametangaza kuwa bei ya dizeli itapungua kwa shilingi 10 kwa lita katika marekebisho yajayo ya bei ya mafuta ya Juni–Julai.

Akihutubia taifa kutoka Ikulu ya Mombasa, Rais amesema hatua hiyo inalenga kupunguza makali ya gharama ya maisha kwa wananchi, wafanyabiashara na sekta ya usafiri.

Amesema serikali tayari imetumia shilingi bilioni 13.7 katika kudhibiti bei ya mafuta kufuatia mzozo wa kimataifa uliosababisha kupanda kwa gharama za mafuta duniani.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *