WALIOPORA MALI NA KUHARIBU WATAANDAMWA, ASEMA MURKOMEN
Waziri wa usalama Kipchumba Murkomen ameonya kuwa waliohusika katika kupanga na waliopora mali wakati wa maandamano ya hapo jana watabeba msalaba wao.
Ameahidi kuhakikisha kuwa walioathirika wakiwemo wanasiasa na maafisa wa serikali na wafanyibiashara wanapata haki.
Murkomen anasisitiza kuwa maandamano ya hapo jana yalikuwa yamepangwa na lengo la kutekeleza uharibifu na kuwa waliofanya hivyo lazima waajibike.
Imetayrishwa na Antony Nyongesa
English 























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































