KALOMBOTOLE KUZUILIWA HOSPITALINI MBAGATHI
Mshukiwa wa mauaji ya wagonjwa 2 katika hospitali ya Kenyatta Kennedy Kalombotole atazuiliwa katika hospitali ya Mbagathi.
Ni uamuzi uliotolewa na hakimu wa mahakama ya Kibera Daisy Mutai anayesema mshukiwa hawezi kuzuiliwa katika kituo cha polisi kutokana na matatizo ya akili aliyo nayo.
Mutai ameelezea haja ya Kennedy kuwa chini ya uangalizi wa wahudumu wa afya kufuatia ombi lililowasilishwa na mawakili wake.
Imetayarishwa na Maureen Mukhobe
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































