PITISHA BAJETI KOMBOA KENYA KUTOKA KWA MADENI ASEMA KIMANI KURIA
Wizara ya fedha imeitaka bunge la kitaifa kupitisha mswada wa fedha bila kuufanyia marekebisho ili kuwezesha serikali kulipa madeni ambayo yamefikia shilingi trilioni 11.2
Kwa mujibu wa Waziri wa fedha Njuguna Ndugu ni kupitia kodi kenya itaweza kupunguza madeni inayodaiwa na mataifa mengine
Tayari kamati ya fedha na mipango ya bunge la kitaifa imeanza kuandika ripoti yake ambayo inatarajiwa kuwasilisha bungeni wiki ijayo
Mbunge wa Molo Kimani Kuria ambaye ni mwenyekiti wa kamati huyo ameahidi kwamba maoni ya wakenya sharti yapewe kipaumbele katika ripoti hiyo
Imetayarishwa na Janice Marete
English 

























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































