SERIKALI ITUPE BOTI ZA BURE ENEO LA GARSEN-LAMU

Uchukuzi umelemazwa katika barabara kuu ya garsen -lamu baada ya mto tana kuvunja kingo zake na kusababisha mafuriko makubwa.
Inaarifiwa kuwa hali hii imewalazimu baadhi ya wanafunzi wanaorejea shuleni kutumia boti kusafiri hadi Mombasa na maeneo ya kaskazini mashariki ya nchi.
Wasafiri wanaotumia barabara hiyo wakilazimika kugharamikia zaidi nauli ya waendako.