HATUNA PESA ZAIDI YA MILIONI 391 ZA KUWAPA KAUNTI

Kamati ya bajeti katika bunge la kitaifa imetupilia mbali pendekezo la seneti kuipa kaunti shilingi bilioni 415 Katika bajeti taifa halina uwezo wa kutoa Zaidi ya shilingi 391.
Mwenyekiti wa kamati hiyo Ndindi Nyoro amesema iwapo wabunge wataidhinisha pendekezo la seneti basi itawalazimu kupunguza bajeti ya hazina ustawishaji maeneo bunge NGCDF.
Ni pendekezo lililoibua mjadala mkali baadhi ya wabunge wakiunga mkono kamati ya bajeti huku wengine wakipinga vikali na kushinikiza kaunti kuongezewa mgao.
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































