MENEJA WA U17 ATAJA KIKOSI CHA MWISHO
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya soka kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17 William Muluhya ametaja kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 25 kitakachoiwakilisha Kenya katika mashindano ya AFCON ukanda wa CECAFA yatakayoandaliwa nchini Ethiopia baadaye mwezi huu.
Vijana hao wa Junior Stars wamewekwa kwenye Group A, Pamoja na wenyeji Ethiopia, South Sudan, Somalia na Rwanda, timu 2 zikiratibiwa kushiriki AFCON mwaka ujao.
Kikosi hicho kinachowajumuisha wachezaji kutoka shule mbali mbali na mchujo wa kambi za kitaifa, kitaondoka nchini hii leo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































