MENEJA WA U17 ATAJA KIKOSI CHA MWISHO
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya soka kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17 William Muluhya ametaja kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 25 kitakachoiwakilisha Kenya katika mashindano ya AFCON ukanda wa CECAFA yatakayoandaliwa nchini Ethiopia baadaye mwezi huu.
Vijana hao wa Junior Stars wamewekwa kwenye Group A, Pamoja na wenyeji Ethiopia, South Sudan, Somalia na Rwanda, timu 2 zikiratibiwa kushiriki AFCON mwaka ujao.
Kikosi hicho kinachowajumuisha wachezaji kutoka shule mbali mbali na mchujo wa kambi za kitaifa, kitaondoka nchini hii leo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 







































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































