KENYA KULENGA NAKISI YA BAJETI YA 4.9% YA PATO LA TAIFA KATIKA 2026/27
Kenya inalenga kiwango cha chini cha bajeti ya asilimia 4.9 ya Pato la Taifa katika mwaka wa fedha wa 2026/27 wa Julai hadi Juni, kulingana na wizara ya fedha.
Imebainika kuwa taifa la kenya limekuwa likipambana na ulipaji wa deni kubwa katika miaka ya hivi karibuni baada ya kuzidisha ukopaji katika kipindi cha tangu 2013 ili kufadhili miradi ya miundombinu, na kulazimisha serikali kujaribu kudumisha njia ya ujumuishaji wa kifedha.
Serikali inapaswa kufanya mikakati kabambe ili kuhakikisha inaongeza mapato ya kutosha kwa ajili ya matumizi muhimu, wakati inatimiza wajibu wake wa madeni.hata hivyo kulingana na afisa huyo Serikali inapanga kujaza pengo la bajeti kwa ufadhili wa nje wa shilingi bilioni 241.8 na ufadhili wa ndani wa shilingi bilioni 775.8.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 










































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































