#Local News

KILIO CHA WAFANYABIASHARA TOI

Wafanyibiashara wa mitumba katika soko la Toi, mtaani Kibera, jijini Nairobi wameibua wasiwasi kuhusu hasara wanayopata  kutokana na kodi wanaotozwa  kila wakati wanaponunua bidhaa.


Wamelalamika madai ya kunyanyaswa mara kwa mara na maafisa kutoka katika
serikali ya kaunti ya Nairobi, hali wanayosema imechangia wenzao kuacha
biashara.


Hata hivyo, wakiongozwa na Philp Wambua, wamelalamikia changamoto zikiwemo viwango vya juu vya kodi, mazingira mabovu ya kazi na ukosefu wa taa za barabarani.

Aidha, wafanyabiashara hao wamelazimika kuongeza bei kwa bidhaa zao, hali
wanayosema imepunguza mauzo kutokana mapato ya chini ya wanunuzi.


Sasa wameitaka serikali kuu kuboresha uchumi, mbali na kuimarisha usafi wa mazingira usalama katika soko hilo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

KILIO CHA WAFANYABIASHARA TOI

PROFESA MUTUA: POKEENI FIDIA

KILIO CHA WAFANYABIASHARA TOI

BODA WAANGUKIWA NA MASHARTI MAGUMU

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *