RUTO AWAPA MAGAVANA JUKUMU
Rais William Ruto amewataka magavana kuhakikisha hospitali zote za umma na za kibinafsi kwenye kaunti zao zimejiandikisha chini ya bima ya afya SHA ili kuhakikisha mpango wa serikali wa utoaji huduma za afya kwa wote UHC unatekelezwa kikamilifu.
Rais ameyasema haya kwenye mkutano na magavana katika Ikulu ya Nairobi hapo jana, akitaja hatua ya baadhi ya hospitali hizo kukosa kujiandikisha kama kikwazo kwenye mpango huo wa serikali.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































