#International

MUSEVENI AONGOZA MATOKEO YA AWALI UGANDA

Rais mkongwe wa Uganda, Yoweri Museveni, ameongoza kwa mbali katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa urais, huku kukiwa na taarifa kinzani kuhusu visa vya vurugu vilivyoripotiwa baada ya kura kupigwa.

Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na tume ya uchaguziMuseveni ana asilimia 76.25 ya kura kulingana na kura zilizohesabiwa kutoka karibu nusu ya vituo vya kupigia kura.

 Mpinzani wake mkuu, mwanamuziki maarufu Bobi Wine, amepata asilimia 19.85, huku kura zilizobaki zikigawanywa miongoni mwa wagombea wengine sita.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

MUSEVENI AONGOZA MATOKEO YA AWALI UGANDA

OMTATAH APINGA UFADHILI WA SHIF

MUSEVENI AONGOZA MATOKEO YA AWALI UGANDA

ODM YAZINDUA ZIARA ZA KAUNTI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *