RUTO AONYA WACHAFUZI WA NAIROBI RIVER

Rais William Ruto ametangaza onyo kali dhidi ya kampuni na watu binafsi ambao wamekuwa wakitupa taka ndani Nairobi River, akisema watawajibishwa kisheria.
Akizungumza mtaani Korogocho jijini Nairobi wakati wa uzinduzi wa usafishaji wa mto huo, Rais amewaonya watakaokiuka agizo hilo kuwa tayari kuwajibikia mienendo yao.
Aidha, ameahidi kwamba nafasi 200000 za ajira zitabuniwa chini ya mradi huo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa