#uncategorized

WAKENYA WACHUNGULIA IEBC MPYA

Mchakato wa kubuniwa upya kwa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC umepiga hatua kubwa, Rais William Ruto akipokezwa rasmi ripoti ya jopokazi lililoendesha zoezi la kuwapiga msasa wanaowania kuhudumu kama mwenyekiti na makamishna wa tume hiyo.

Akizungumza katika Ikulu ya Nairobi, Rais Ruto amelipongeza jopokazi hilo, akiahidi kuhakikisha wanaoteuliwa kuhudumu ni watu walio na vigezo hitajika.

Jopokazi hilo linaongozwa na mwenyekiti wake Dakta Nelson Makanda.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WAKENYA WACHUNGULIA IEBC MPYA

RUTO AINGIA SOUTHRIFT

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *