UHABA WA MATABIBU WAATHIRI HUDUMA ZA AFYA
Uhaba wa matabibu nchini umeathiri huduma za afya kwa wakenya serikali ikitakiwa kuajiri wahudumu hao Zaidi.
Wakiongea kwenye kongamano linaloendelea huko Mombasa wanasema idadi ya wagonjwa wanaohudumiwa na tabibu mmoja iko juu zaidi ikilinganishwa na kiwango kilichowekwa na shirika la afya duniani WHO.
Wanasema kutokana na uhaba huo wagonjwa mara nyingi hutumwa katika vituo vingine vya afya hali inayochangia magonjwa wanayougua kukosa kushughulikiwa kwa wakati.
Imetayarishwa na Maureen Mukhobe
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































