#Local News

WATATU WALIOTOWEKA WAKATI WA MAANDAMANO WAPATIKANA KAJIADO

Watu watatu waliotoweka wakati wa maandamano ya Kitengela kaunti ya Kajiado ambao ni ndugu wawili na mwanaharakati mmoja, wamepatikana wakiwa hai

Watatu hao walitoweka tarehe kumi na tisa mwezi wa Agosti mwaka huu, wakati wa maandamano ya Gen Z ya kuishinikiza serikali iliyoko mamlakani kufanya mageuzi na kupunguza gharama ya Maisha. Gen Z walijitokeza pia kupinga sera za utawala wa Kenya Kwanza

Rais wa chama cha mawakili nchini, LSK, Faith Odhiambo amedhibitisha ndugu hao Jamil and Aslam Longton, wamepatikana katika eneo la Gachie kaunti ya Kiambu, naye Bob Njagi akipatikana pia akiwa hai eneo la Tigoni pia huko Kiambuu. Baba yake Longman Njagi amesema alipigiwa simu usiku na polisi wa Tigoni, wakimfahamisha kwamba Bob yuko hai.

Imetayarishwa na Kennedy Osoro

WATATU WALIOTOWEKA WAKATI WA MAANDAMANO WAPATIKANA KAJIADO

MAHAKAMA KUTOA UAMUZI KUHUSU INSPEKTA MKUU WA

WATATU WALIOTOWEKA WAKATI WA MAANDAMANO WAPATIKANA KAJIADO

WABUNGE KUPINGA KUPOKONYWA DONGE LA NG-CDF

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *