KENYA U-20 KUKABILI KUNDI GUMU AFCON MISRI
Timu ya taifa ya vijana wa chini ya miaka 20 itakabiliana na Nigeria, Tunisia na Morocco kwenye kundi gumu katika michuano ya AFCON ya mwezi huu nchini Misri.
Kenya, chini ya kocha Salim Babu, itashiriki kwa mara ya kwanza huku wapinzani wao wakiwa na uzoefu mkubwa.
Nigeria ni mabingwa mara saba na wamewahi kushiriki Kombe la Dunia la U-20 mara 13.
Morocco walitwaa taji lao pekee mwaka 1997, huku Tunisia wakimaliza nafasi ya pili mwaka 1985 na ya nne mara mbili, ikiwemo kupigwa 4-0 na Nigeria mwaka jana.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































